ALFU LELA U LELA
AU
USIKU ELFU NA MOJA
HAPO KALE paliondokea Sultani mmoja wa ki-Sassanid aliyekuwa
na enzi kubwa iliyoenea toka Bara Hindi mpaka
Uchina. Jeshi lake kubwa lenye nguvu,
liliweza kuishindi na kuiteka kila nchi
ya jirani na sifa za utawala wake zikaenea
kila pembe ya dunia. Alipofariki,
akawaacha wanawe wawili waliokuwa
mashujaa na hodari wa kupanda farasi,
hasa mkubwa aliyeitwa Shahriyar
aliyerithi kiti cha enzi cha baba yake.
Yeye alifuata nyayo za baba yake
mpaka raia zake wote wakampenda.
Mdogo wake aliyeitwa Shahzaman
akawa Sultani wa nchi ya Samarkand.
Basi hawa wana Sultani wawili
wakaendelea kutawala nchi zao
kwa furaha na kwa haki kwa muda
wa miaka ishirini mpaka siku
moja Sultan Shahriyar akaingiwa
na hamu kubwa ya kutaka kumwona mdogo
wake. Basi akamwamuru Waziri wake
aende Samarkand akamwalike.
Waziri akafunga safari. Baada ya safari ndefu ya siku nyingi katika jangwa, mbuga na nyika, akawasili katika mji mkuu wa Samarkand.
Bila kuchelewa akafikishwa mbele ya Sultan Shahzaman aliyefurahi sana kupokea salamu na ujumbe kutoka kwa kaka yake. Naye bila kuchelewa akatoa amri safari ya kumzuru kakiye itayarishwe. Akatanguliza msafara wa ngamia na farasi ulioshehenezwa vyakula na zawadi ukiongozwa na watumishi na wajakazi wake wa kumhudumia wakati wa safari yake ndefu. Kabla hajaondoka, akamchagua Waziri wake mkuu amshikilie madaraka yake mpaka atakaporudi. Matayarisho yalipokamilika, msafara ukang´oka.
Usiku Sultan Shahzaman akakumbuka amesahau zawadi muhimu aliyodhamiria kumpa kaka yake. Basi bila kuonekana na yeyote, akatoka hemani mwake akarejea kwenye kasri lake. Alipoingia ndani, lahaula!
Akamkuta mkewe amekumbatiwa kimapenzi na mtumwa wake mmoja! Kuona vile, akapigwa na bumbuazi na mshangao mkubwa. Hakuweza kuamini yale aliyokuwa akiyashuhudia pale penye sofa! Akafikiri: "Kitendo kama hiki kama kinaweza kutokea wakati sijafika mbali, iblisi huyu atafanya nini nitakapotoweka mbali?" Hapo akafuta upanga wake, akawaua wote wawili pale pale.
Endeleya!
Copyright © 2001 2002 Mombasa Web, Inc. All rights reserved..