Site hosted by Angelfire.com: Build your free website today!

[Mwanzo]    Rudi table

 

[Vituko Vya Bibi Huyu - Eddy Sheggy]

Nikitazama milima ya kwetu eeee, 

machozi yanitoka kwa uchungu na mawazo

Tulitoka wawili ninarudi peke yangu,

Baba na Mama wataniuliza Bibi yako yuko wapi

Natamani gari lisifike upesi, 

kwa ile aibu nitakayo pata mbele ya wazazi

Kwa vile miezi michache imepita nilitoka na bibi yule

 

Alianza kuweka chumvi kwenye chai, 

nilikua na wageni wakatoka bila kuaga

Akaweka sukari kwenye mboga, 

nikaonja haviliki tukalala na njaa

Juzi juzi kavunja kioo cha dirisha, 

apate kuchungulia wapitao njiani

 

Walisema dalili ya mvua ni mawingu

Niliyempenda kanitoroka maa

(Kanitoroka nateseka) Walisema.........

 

[Sheggy]

Vituko eee vituko vya bibi huyu.......................

Sitaweza kumsahau oo mama aa

Sitaweza kumsahau oo bibi eeee

Alikua kama Helkopta, 

ndege isiyochagua mahali pa kutua ee

Kila mtaa hapa jijini tazameni oh

Hana bwana mmoja wala wawili nifanye nini oh mama aa

 

 

(Walisema.............................)

 

Rudi mwanzo

 

[MOYO FICHO LA SIRI- BENDI(SHEGGY)]

Ama kweli moyo ni ficho la siri mama

Ningelijua nisingempa penzi langu loote nimeeangaika mama

Kupoteza wakati wangu bure oo mama

Kusahau wapenzi wangu woote..ooo mama..sababu yake bety,

oo..mama ee mama..ee bety

sikumoja nilipokuwa nikimsindikiza Shangazi yangu air port nilishangaa,

Kumkuta Bety eee,akimpokea rafiki yangu katokea masomoni 

Nillishikwa na butwaaa aliponijulisha ya kwamba eti ni mchumba wake katokea masomoni.

Nimeachwaa ninashangaaa,mwenzenu nalia sheggy

 

(Chorus)

ooh najuta Sheggy ,najuta ooh kumpenda Cathy

oooh Sheggy najuta ooh kumpenda Cathy,

Nayakubali ya kale,asiyekubali kushindwa si mshindani mama..oooh ...mamaoooh x2

(rudia chorus)

 

Rudi mwanzo