Site hosted by Angelfire.com: Build your free website today!

[Mwanzo]        Rudi Table

[Anifa - Makassy ]

Mtoto wa Arusha mama mbona wanipa shida

Mimi ni wako waikana mulu eee

Wache waseme seme watachoka wao 

(Chorus)

Mapenzi ya pesa hayadumu Mama
Mapenzi ya roho ni ya maisha

Nimekupenda na wewe umekubali

Ukila kisamvu.......ooooooo

Kaza roho Mama
DAR-ES- SALAAM jiji umbeya mwingi

[Rudi mwanzo]

[Athumani - Makassy]

[Wote]
 
Athumani eee vipi mambo VALUVALU?
 
Umenioa bado ningali kijana
 
Ukipata chungu kipya usitupe cha zamani.........Athumani eee
 
 
 
Athumani eee samaki apishe chambo
 
Kila apitae Athumani asabahi
 
Kusema sema sijui kubishana sitaweza........Athumani eee
 
(repeat x 3)
 
 (Chorus)
 
[Wote]
 
Mke wa ne eee.....mke wa ne...
Unkasigo oooh, unkasigooo
Akana ubufi nu bumi,
Atikulonda ukwendenda,
Akamanya kuyelayela,
Atugalile kanunu fijoooooo!

[Rudi mwanzo]

 

[Umasikini Si Kilema - Makassy]

 

Umasikini si kilema ni matatizo

Ni matatizo ya Dunia ndugu yangu

Kitu kimoja ninalia watoto wangu...

Wamenikimbia kwa sababu shida nyingi

 

Kuku anakula sawa na mdomo wake....eee

 

(Chorus)

 

Yaliyopita nayo yamepita

Yatayokuja nayo yatapita

Aaaa Aaaa Aaaaaaaaa

 

Rudi mwanzo

 

[Bomoa(tutajenga Kesho) - Makassy]


Bomoa ee bomoa ee bomoa mama tutajenga kesho
Tutajenga kesho imaaa
 
[Mmoja]
Nyinyi watoto wazuri wote njooni tucheze leo
Bomoa eee
 
[Wote]
Bomoa, bomoa, bomoa mama.....  

 

[Rudi mwanzo]

 

[Siku Ya Kufa - Makassy Orchestra] - tizedboy 


[Prelude miondoko ya kulonga]
Hii nyimbo ni nyimbo ya ukumbusho
Wa siku ya kuzaliwa na siku ya kufa
Tumetoka kwa udongo....
Tutarudi kwa udongo
 
[Mwanzo----Remmy]

 

Mawazo mawazo ya mutu muzima ee
Kila akikuambia neno usibishe ee
Ila ya muzee ukabisha mwisho utapata tabu
 
Kuimba tunaimba nashauri musikie
Ila msisahau muziki ya Makassy inawasuhia
Mambo yenye manufaa

 

Siku ya kufa siku ya kufa siku ya kufa
wandugu kwaheri
Siku ya kufa nyama ya udongo
 
Akina Mama kwaheri
Dar Internationale kwa heri
Marquis kwa heri
Supa Afrika kwa heri
Dar es Salaame kwa heri


 
Piga hodi utafunguliwa ee
Maiti haina rafiki
 
Mwanamuke muzuri hakosi kasoro ooooo
 
Mwendo wa chura kuruka ruka e
Mwendo wa bata upande upande
 
Mwendo wa Jongoo kusua sua e.......atafika tu!
Jongoo mpenda watu e na watu hawamupendi Jongoo oo Jongoo

 

[Mwanangu Celina - Makassy Orchestra] - tizedboy
 
Mwanangu Celina, mbona hutulii
Hali yako eee
Si ya kawaida
Hata chakula huli vizuri
Sababu gani Mwanangu eee
 
[Mmoja]
Baba nashukuru kuniuliza swali kama hilo
Nilipokuwa Shuleni, uliniambia nimalize kusoma
Masomo nimemaliza
Leo hii ni miaka mitatu
Nitafute Kazi
Hutaki unataka niolewe!
 
Nimepata ee atayenifaa
Nimempata ee wangu wa milele oooo
Mama mama ma a
 
[Wote]
Mwanangu Celina.........

 

[BINADAMU HATOSHEKI - Makassy Orchestra] - Mtukwao
 
 
Kwa vipi atatulia jaaamani,
Ikiwa apatacho hakimtoshi,
Awe ni mwenye mali,
Ataka tena nyingine,
Kulalamika hachoki yeee,
Binadamu kweli hatosheki.
 
 
Kibwagizo:
 
EEh jamani eeeh ,binadamu hatosheki,
Hata ukimpa , nini  
Milele hatoridhika,
 
 
Leo mvua inanyesha, binadamu achukia,
Kesho jua linawaka, binadanmu achukia eeeh,
 
Eeeeh amani eeeh, binadamu hatosheki,  
Hata ukimpa nini, milelel hatoridhika eeeh
 
Ukimpa tano leo,kesho atataka kumi
 
Eeeh jamani ,binadamu ......