Site hosted by Angelfire.com: Build your free website today!

[Mwanzo]        Rudi Table

[Baraka - Kimulimuli]

 
Jana jioni, tulimaliza sherehe,
Sherehe za harusi,
Alipoolewa dada,
Na mume ampendaye,
Na Mungu awabariki,
Waje wapate watoto,  
Wa kike na wa kiume,
Diana  dada hongera sana!
 
Kibwagizo:
 
Kazi uliyofanya, Dia dada kazi kubwa,
Kwani vijana wa sasa hawapendi kuoa,
Nao akina dada hawapendi kuolewa,
Iliyobaki ni sisi ndio tunatia nguvu,
 
 
Twawaombea baraka, ( baraka kwa Mungu eeh)x2
Baraka kwa Bwana Mungu eeeh ( baraka kwa Mungu)x2

[Rudi mwanzo]

 

[Kisa Cha Foto Album - Kimulimuli]

[Wote]

Wameniambia mambo yako mama eee

Wamenieleza matatizo ya mume wako eee

Na kisa cha we Sheri Zinduna kufika kupewa TALAKA!

 

Wameniambia mambo yako mama eee

Wamenieleza matatizo ya mume wako eee

Japo mwenyewe hukutaka wanambie siri yako moyoni

 

Foto Album inaleta maneno katikati ya mji wa Mwanza

Kisa ni picha ilopigwa zamani katikati ya Dar-es-Salaam'a

(repeat)

 

(Chorus)

[Wote]

Sheri Zinduna nakupa pole Zinduna eee

Sheri Zinduna nakupa pole Zinduna eee

 

[Zahir]

Matatizo yanakukuta

Mkasa nyumbani kwako eee

Ndoa imevunjika mama eee kosa ni picha ya zamani ooo

 

[Wote]

Sheri Zinduna nakupa pole Zinduna eee

Sheri Zinduna nakupa pole Zinduna eee

 

[Zahir]

Afadhali ngekuwa labda mie nimewahi kufika Mwanza

Lakini toka nimezaliwa ee.....

Sijafika Mwanza aaa

 

[Wote]

Sheri Zinduna nakupa pole Zinduna eee

Sheri Zinduna nakupa pole Zinduna eee

 

[Zahir]

Kipato baba watoto ajue sijafika Mwanza ee....

Toka mimi nimezaliwa ee

Vitongoji navisikia kwa watu eee

 

[Wote]

Sheri Zinduna nakupa pole Zinduna eee

Sheri Zinduna nakupa pole Zinduna eee

 

[Zahir]

Kitongoji cha Nyama nacho...

Pamoja na Kirumba nasema

Kigogo na Isamba eee

Nimeelezwa na wenyeji aaa

 

[Wote]

Sheri Zinduna nakupa pole Zinduna eee

Sheri Zinduna nakupa pole Zinduna eee

 

[Zahir]

Ni sawa sawa ya Kanuta ee

Pamoja na Miti Mirefu mama ee

Pamoja na mtaa wa Sukuma ee

Wamenambia wenyeji aaaaa....

 

[Wote]

Sheri Zinduna nakupa pole Zinduna eee

Sheri Zinduna nakupa pole Zinduna eee........

[Rudi mwanzo]

[Kabwe Part I - Kimulimuli]


Ulipokuwa ukikanywa, hukutaka kusikia,
Ile tabia mbaya, hukutaka kuibadilisha,
Dunia ya Mungu, sasa inakufunza,
Fungua macho ,
jaribu kujirekebisha Kabwe x2


Kila hila wazazi wako waloitumia,
Katika kukufundisha, ulizidi kuwa mtukutu,
Baba alipokukanya , ulizidi kuwa mtukutu,
Mama alipokukanya , ulizidi kuwa mtukutu,
Walimu wa shuleni kwenu Kabwe ukitaka kupigana nao,
Yote yanayokukuta, wa kulaumu ni we mwenyewe x2

Tabia ya udokozi Kabwe ulianza siku nyingi,
Wakubwa kubadilika, sasa ni jangili mkubwa weeex2


Habari zako zote, zinafika kwetu eeh,
Hatuji kukuona gerezani, si kama si tumekususa,
Watuona kimya, kazi zimetuzidi,
Kazi zimetuzidi ,kazi za ujenzi wa taifa letu changa x2

 

Rudi mwanzo

 

[Kabwe Part II - Kimulimuli]

Kabwe rudi nyumbani,
Ukitoka gerezani,
Uje ujiunge nasi,
Sote tushiriane,
Kulijenga Taifa, Taifa letu hili changa Kabwe x2

Kibwagizo:

Kabwe yoyoyo,
Kabwe mwana kwetu karibu nyumbani oooh x2

Karibu Kabwe karibu,
Karibu kijijini,
Karibu Kabwe karibu,
Karibu kwetu Likwini,
Karibu mwana kwetu, kwenu ulikozaliwa Kabwe!

Kabwe katoka kwenye chuo cha mafunzo,

Wala hakutaka kurudia kwapukwapu
[Kama zamani yooo]

Karibu Kabwe karibu .....

Rudi mwanzo

 

[Wazazi - Kimulimuli]


Wazazi, wazazi wetu eee
Mashujaa tuliorudi, tumerudi kishujaa
Mashujaa walokufa wamekufa kishujaa
Lengo na nia yetu wazazi lilikuwa moja
Kuilinda hadhi yetu eeh

[Mmoja]
Tulipofika ...... na akachamaa
Tulipofika Entebe na akachamaaa .....

 

Rudi mwanzo

 

[Kitu Mapenzi - Kimulimuli]

 
Kitu mapenzi kilianza zamani,
Toka wakati wa mababu zetu,
Na hata wao mapenzi waliyakuta,
Tokea enzi za Adamu na Eva,
Yalianza zamani nasi tuliyakuta x2
 
 
Inasemekana zamani sana,
Katika ile bustani maalum ya Eden,
Chui na mbuzi walikula pamoja,
Tohe na simba walishirikiana
 
Sote tu binadamu Christina elewa,
Ni aibu sana kwa tabia zetu,
Christina ahadi!
 
Kama ni kutengana tutenganishwe na kifo,
Hata huo sio mwisho tutakuja kukutana,
Tutakutana tena kesho kwenye Paradiso

Rudi mwanzo

 

[Moto Ni Moto - Kimulimuli]

 

 

Unatega masikio kusikiliza fitina mama

Dunia hii ya Mungu, watu ni wa aina nyingi mama

Wengine hawana huruma mama

 

Wanafanana na moto

 

Wacha kucheza na moto

 

Moto ni Moto huunguza

Rudi mwanzo

 

[Uzuri Wa Tausi - KIMULIMULI]

 

[Prelude]

Aaa ni maneno ya ugombanishi, ni maneno ya kuvunja nyumba

Aa shoga yangu unataka kunitenganisha na mume wangu

Nakupasha nimeshituka

Nimeshituka...

 

[Vyombo na mwanzo wa nyimbo]

 

Shoga leo nisikilize

Shoga leo nikupashe

Na urafiki wetu utakwisha leo

Nakuona una nia mbaya

Uje uniachishe kwa mume wangu.......

Oh shoga yangu eeeee

 

Shoga we ulisema maneno mengi

Lakini haya ya leo nashindwa kuvumilia

Naona mwisho nitakuja achwa....

Uje kunicheka aaaa

 

Shoga ni wewe uliyesema

Kwa kuwa mume wangu ni mwana miziki....

Kama kweli ananipenda....

Angeniimba kwenye nyimbo zake...

Na kunifananisha na ndege Tausi....

Oh shoga yangu eee

 

Shoga sasa nitakupasha...

Nywele za Tausi hazitaji kitana

Mguu wa tausi hauhitaji kiatu

Macho ya tausi hayapakwi wanja

Mimi ni binaadamu tausi ni ndege.....

Uzuri wake nitaupata wapi ?.....

Tausi mwenye rangi eee

 

[Zahir]

Umempasha vya kutosha mama ooooo

Atazaaame ustaarabu wa kwake yoyoyoyo

 

Umempasha vya kutosha mama ooooo

Atazaaame ustaarabu wa kwake yoyoyoyo

Asifate mambo yasiyomuhusu

Atazaaame ustaarabu wa kwake yoyoyoyo

 

Na kama kukusifu we mama watoto

Hilo ni jukumu langu

Na sasa naamua.....

 

 

[Wote]

Mama watoto pasenti mia moja

 

[Zahir]

Kwa ukarimu kwa wageni wetu nyumbani mama oooo

 

[Wote]Mama watoto pasenti mia moja.....

 

Rudi mwanzo

 

[TIKISA - Kimulimuli(Zahiri Ally Zoro)]

 

Tikisa amerudi salama kutoka Paris,......

Tikisa ana mambo ,tikisa huyu azungumzi kiswahili i!

Salam yake ni Bonjuu mensier! bonjour!

Savaur? savaa byee!

 

Chorus:

Hata siku moja uje kuwachukua mkeo na watoto wako ehee!

Watoto mali yako ni jasho lako maua!....

...........

Siku moja tikisa alijaribu kumrubuni mwanafunzi kwa kifaransa.............

Ikamkuta aibu yule dada alipojibu!

Excee mwa!

communicae mwa in kiswahili,kigogo kizaramo.....

 

Rudi mwanzo

 

[Chiku - Kimulimuli]

 

Nimekubali yanayosemwa na watuuu,

Ni kweli anayependwa na wengi siku zote hufa angali kijana x2

Chiku wangu wee, kalale pema peponi

Chiku wangu weee, daima nitakukumbuka

 

Fadhila na Rehema binti zetu, nitawatunza, nitawalea ipasavyo, naahidi mbele yako

Hawatapata taabu hata siku kwa ukumbusho kwa mapenzi yetu

 

Chiku wangu weeee

[Rudi mwanzo]

[Oliva - Kimulimuli] 
 
Oliv mama,
Mwana kwetu eeeh,
Sikiliza Oliva,
Nikupashee,
Nilipokutana nawe,
Japo mara ya kwanza,
Tabasamu lako,
Lilishika pendo langu,
Oliva, mama yoooo,ooh, ohhh x2
 
Kibwagizo:
 
Tutakapokubaliwa,
Tutafunga ndoa Oliva wangu,
Tutafunga ndoa Oliva wangu, x2

[Rudi mwanzo]